Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2000-2005 | Session 12 | Sitting 7 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 118 | 2025-02-05 |
Name
Rehema Juma Migilla
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuruhusu maeneo ya hifadhi yaliyokosa sifa yatumike kwa matumizi ya kilimo na makazi?
Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia maelekezo ya Serikali imefuta mapori tengefu 12 yenye ukubwa wa ekari 707,962 kwa Tangazo la Serikali Na. 427/2020 yaliyokosa sifa na kurejeshwa kwa wananchi, kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Wizara imefuta hifadhi za misitu saba zenye ukubwa wa ekari 46,715 kwa Tangazo la Serikali Na. 544/2020 zilizokosa sifa na kurejeshwa kwa wananchi, kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo makazi na kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hatua nyingine Wizara imetekeleza uamuzi wa Baraza la Mawaziri kwa kumega takriban ekari 973,380.906 kutoka katika maeneo ya hifadhi za Taifa, mapori ya akiba, mapori tengefu na hifadhi za misitu, kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya wananchi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved