Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 66 2016-09-13

Name

Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSANNE P. MASELLE aliuliza:-
(a) Je, Serikali imechukua juhudi gani za makusudi kudhibiti vitendo vya kubambikizia watu kesi vinavyofanywa na baadhi ya askari wasiokuwa na maadili?
(b) Je, Serikali itakuwa tayari kuanzisha kitengo cha siri ndani ya Jeshi la Polisi kitakachoshughulikia adha hii?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susanne Maselle, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni, miongozo pamoja na taratibu na wale wanaobainika kukiuka maadili ya Jeshi, huchukuliwa hatua kwa kuwashitaki kijeshi kwa mujibu wa PGO 103 na 104 kwa kuwapa adhabu mbalimbali ikiwepo kuwafukuza kazi anaobainika kukiuka maadili ya Jeshi ikiwemo kubambikia watu kesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imefanya jitihada za kuanzisha Kitengo cha Malalamiko katika ngazi ya Makao Makuu, Mikoa na hata Wizara ili kutoa mwanya kwa mtu yeyote anayeona kuwa ameonewa, kuwasilisha malalamiko yake na malalamiko hayo kushughulikiwa. Hata hivyo, raia wanayo haki ya kulalamika katika vyombo vingine vya kisheria wanapoona hawatendewi haki kwa mujibu wa sheria za nchi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi limeweka wazi utaratibu wa namna ya kuwashughulikia askari wasio waaminifu, hivyo halitakuwa tayari kuanzisha kitengo cha siri kwa kazi hiyo kwani utaratibu uliopo unashuhudia na umekuwa na mafanikio.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, siku za usoni kama hivyo ilivyo kwa mikoa michache hapa nchini ambapo kazi ya polisi itabaki kuwa ni ya kupeleleza kesi na mwenye mamlaka ya kupeleka kesi mahakamani ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali. (Makofi)