Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 12 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 213 | 2025-02-12 |
Name
Constantine John Kanyasu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-
Je, lini Wananchi wa Kata za Kasamwa na Nyamkumbu - Geita Mjini watalipwa fidia kutokana na alama za barabara kuwekwa katika maeneno yao?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wananchi wa Kata ya Kasamwa na Nyankumbu waliowekewa alama za X ya kijani ni wale ambao wamo katika eneo la hifadhi ya barabara lililoongezwa kutoka meta 22.5 hadi mita 30 kila upande kulingana na Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007 na Kanuni zake za mwaka 2009.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa uchambuzi wa kina unafanyika ili kubaini ni barabara zipi kweli zinahitaji upana wa eneo la hifadhi ya barabara wa mita 60 kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na hapo baadaye ya kuzipanua kulingana na ongezeko la wingi wa magari. Zoezi hili likikamilika taarifa ya Serikali itatolewa. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved