Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 26 2025-04-09

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa Km 231 utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa kilometa 225.8 umekamilika. Ili kurahisisha kazi za ujenzi, barabara hii imegawanywa katika sehemu tatu, sehemu ya kwanza ni Nangurukuru – Zinga yenye urefu wa kilometa 78.7, sehemu ya pili ni Zinga – Choya (kilometa 71.4) na sehemu ya tatu ni Choya – Liwale (kilometa 75.7).

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya usanifu kukamilika, Serikali imeanza ujenzi wa sehemu ya tatu ya Liwale – Choya (kilometa 75.7) ambapo zabuni kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha kilometa 10 kutoka Liwale kuelekea Choya zimetangazwa tarehe 3 Februari, 2025 na kwa sasa iko katika hatua ya uchambuzi (evaluation). Kazi za ujenzi zinatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Juni, 2025. Kwa sehemu zilizobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuendelea na ujenzi. Ahsante. (Makofi)