Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 10 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 166 | 2025-02-10 |
Name
Neema Kichiki Lugangira
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
Kufikisha Umeme wa REA Mashuleni
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza:-
Je, Serikali haioni haja kupitia upya Mkataba wa REA kuhakikisha umeme unafikishwa mashuleni ili shule ziunganishwe na huduma za TEHAMA?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatoa kipaumbele katika kufikisha umeme kwenye taasisi zinazotoa huduma kwa jamii zikiwemo Taasisi za Elimu. Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma ya umeme wa uhakika katika maeneo hayo. Hadi kufikia mwezi Januari, 2025 taasisi za elimu zilizopatiwa umeme kupitia REA ni 18,597. Aidha, Serikali kupitia REA itaendelea kupeleka umeme kwenye vituo vya huduma nchini kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved