Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 36 | 2025-04-10 |
Name
Justin Lazaro Nyamoga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano Vijiji vya Lukani na Ng’uluhe - Kilolo ili kuboresha mawasiliano?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia UCSAF ilifanya tathmini ya hali ya mawasiliano katika maeneo mbalimbali Wilayani Kilolo mwaka 2021/2022 kwa lengo la kubaini maeneo yenye changamoto ya mawasiliano ya simu. Katika tathmini hii ilibaini uwepo wa changamoto katika Kata za Ibumu, Irole, Uhambingeto, Kimala, Mahenge na Masisiwe. Wizara ilijumuisha Kata hizo kwenye Mradi wa Ujenzi wa Minara 758 katika kata 753 unaotekelezwa kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi katika Kata mbili za Irole na Masisiwe umekamilika na utekelezaji katika kata nyingine nne unaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wizara kupitia UCSAF ipo katika maandalizi ya kutekeleza mradi wa awamu ya kumi, hivyo Kata ya Ng’uluhe hususan maeneo ya Vijiji vya Lukani na Ng’uluhe alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge vitaingizwa katika zabuni hii ya awamu ya kumi ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kufanyika katika mwaka wa fedha 2025/2026. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved