Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 70 2016-02-02

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkokotoni kilichoko Unguja?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkokotoni bado haujakamilika. Hadi sasa kazi ya ujenzi wa kituo hicho imefikia asilimia 80 ikihusisha ujenzi wa jengo lenyewe, kupauwa na kupigia plasta kuta zote. Kazi kubwa iliyobaki ni kufunga milango, madirisha, kuweka sakafu, kupiga rangi na kununua furniture. Serikali inakusudia kumalizia ujenzi wa kituo hicho ndani ya mwaka wa fedha 2016/2017 kulingana na upatikanaji wa fedha za bajeti.