Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 37 | 2025-04-10 |
Name
Deodatus Philip Mwanyika
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa utaanza Mkoani Njombe?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunavyofahamu, Kiwanja cha Ndege cha Mkoa wa Njombe ni muhimu kimkakati hususan kwenye kukuza uchukuzi katika usafiri wa anga kijamii, kiuchumi na kibiashara ikiwemo biashara ya mazao ya misitu, mbogamboga, matunda (maparachichi) ambayo yote hayo huzalishwa na kusafirishwa nje ya nchi. Aidha, kufuatia uboreshwaji wa Shirika la Ndege la ATCL uliopelekea manunuzi ya ndege kubwa ya mizigo aina ya Boeing 767-300 F, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwa kushirikiana na Mkoa wa Njombe imekamilisha uchambuzi wa eneo jipya la TANWAT kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege na sasa Serikali inaendelea na taratibu za utwaaji wa ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Serikali imeidhinisha taarifa za awali za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambapo kiasi cha shilingi milioni 804 zimetengwa kwa mwaka 2024/2025 huku Mtaalamu Elekezi akiendelea na utayarishaji wa rasimu ya mwisho ya nyaraka zitakazotumika kwa ajili ya ununuzi ya mkandarasi atakayetekeleza mkataba wa ujenzi. Mara baada ya kazi hii kukamilika, ujenzi utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa mwaka 2025/2026 Serikali inatarajia kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya Kiwanja hicho.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved