Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 40 | 2025-04-10 |
Name
Kavejuru Eliadory Felix
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Buhigwe
Primary Question
MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga viwanda vya kuchakata zao la migomba?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Zao la Migomba ama ndizi ni miongoni mwa mazao makubwa katika Wilaya ya Buhigwe na maeneo mengine nchini. Kutokana na tafiti zilizofanywa duniani zao la migomba linaweza kutumika kutengeneza bidhaa kama vile vikapu, mikeka, kofia, chakula cha mifugo, mbolea, nguo, karatasi, nyuzi, dawa za asili na malighafi za kujengea lakini pia matunda yake hutumika kama chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) na Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) ina teknolojia ya kuchakata migomba kwa ajili ya chakula cha mifugo na viwanda vya kutengeneza mvinyo, unga wa lishe, keki na crispy zinazotokana na ndizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa uongezaji thamani zao la migomba pamoja na ndizi, Serikali kupitia SIDO imepanga kuanzisha kongani ya zao la migomba na ndizi katika halmashauri, ikiwemo Halmashauri ya Buhigwe ili kuongeza mnyororo wa thamani kwa zao hilo. Aidha, zao hili ni miongoni mwa mazao yatakayoongeza thamani nchini kupitia mpango maalum wa kuendeleza viwanda wa miaka mitano unaotarajiwa kuanza kutekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026 hadi 2029/20230. Nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved