Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 86 | 2025-04-16 |
Name
Stephen Lujwahuka Byabato
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: -
Je, lini Barabara ya Lake Oil - Ijuganyodo hadi Kyamunene itajengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/2025 Barabara ya Lake Oil – Ijuganyodo hadi Kyamunene imetengewa shilingi milioni 40 kwa ajili matengenezo ya changarawe urefu wa kilometa 2.078 na ujenzi wa mifereji mita 800. Aidha, mkandarasi wa kazi hiyo ameshapatikana na anatarajiwa kuanza hivi karibuni. Katika mwaka 2025/2026 barabara hiyo pia imewekwa kwenye mpango wa bajeti kwa kutengewa shilingi milioni 33 kwa ajili ya matengenezo ya kiwango cha changarawe urefu wa kilometa mbili ili kukamilisha urefu wa kilometa 4.078.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved