Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 120 2025-04-23

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kusajili wanafunzi katika shule ya Msingi ya Ushirika Kata ya Mpuguso iliyojengwa kwa nguvu za w ananchi?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Shule ya Msingi ya Ushirika ilisajiliwa rasmi tarehe 9 Januari, 2024 na kupewa namba ya usajili EM.20614, kwa barua yenye kumbukumbu Na. EA.295/315/20A/32 ya tarehe 9 Januari, 2024.

Mheshimiwa Spika, shule hiyo ilianza kupokea wanafunzi tarehe 5 Februari, 2024. Kwa sasa shule ina jumla ya wanafunzi 138, wakiwemo wavulana 74 wasichana 64 ambao wako darasa la awali hadi darasa la tatu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inawapongeza wananchi wa Kata ya Mpuguso kwa michango na jitihada zao zilizowezesha upatikanaji wa elimu karibu na maeneo yao.