Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 128 2025-04-23

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Je, upi mpango wa Serikali wa kulipa madeni ya wazabuni hasa ya Polisi na Magereza?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua madeni wanayodai wazabuni mbalimbali wanaotoa huduma, ambapo kwa Jeshi la Polisi kiasi cha fedha shilingi 651,730,893,477.29 kinadaiwa na katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imelipa kiasi cha fedha shilingi 3,188,596,251.62. Aidha, deni la wazabuni katika Jeshi la Magereza ni jumla ya shilingi 33,527,055,286.00/= na kiasi cha fedha shilingi 15,072,994,270.00 kimefanyiwa uhakiki na Hazina na kinachosubiriwa ni malipo kutoka Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kulipa madeni hayo kwa kadri ya upatikanaji wa fedha toka kwenye bajeti ya Serikali inayotengwa kila mwaka wa fedha. Ahsante.