Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 153 2025-04-28

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. LATIFA KHAMIS JUAKALI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia vijana elimu kuhusu mikopo ya asilimia 10?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikitoa mikopo kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu inayotokana na 10% ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuzingatia Kifungu cha 37A cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290 na Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu za mwaka, 2024.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 38 ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu za mwaka 2024, Mamlaka ya Serikali ya Mitaa zinapaswa kutoa mafunzo kwa vikundi vinavyoomba na kupata mkopo ikiwemo masuala ya uwekaji wa akiba, uundaji wa vikundi vyenye tija, uongozi, usimamizi wa fedha, uendeshaji wa miradi na utoaji wa taarifa na usimamizi wa marejesho ya mikopo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia Kanuni hiyo katika mwaka wa fedha 2024/2025, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimetoa mafunzo kwa vikundi 2,827 vya vijana ambavyo vilipewa mikopo ya 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.