Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 157 | 2025-04-28 |
Name
Nicodemas Henry Maganga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbogwe
Primary Question
MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme wa REA kwa vitongoji ambavyo bado havijapatiwa umeme wa REA Mbogwe?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mbogwe lina jumla ya vitongoji 335 ambapo kati ya hivyo, vitongoji 140 vimepatiwa umeme, vitongoji 82 Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa miradi na vitongoji 63 zabuni imetangazwa ili kupata Wakandarasi wa kutekeleza kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili B. Aidha, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini itaendelea kutenga fedha ili kugharamia utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 50 vilivyosalia. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved