Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 549 | 2025-06-10 |
Name
Maimuna Ahmad Pathan
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga uzio kwa shule zilizopo maeneo hatarishi kwa kuwa shule nyingi za Mkoa wa Lindi hazina uzio?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kujenga uzio katika shule mbalimbali za msingi kwa kuzipa kipaumbele shule zenye watoto wenye mahitaji maalum.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2022/2023 – 2023/2024 Serikali imetoa shilingi bilioni 5.57 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika shule 185 za watoto wenye mahitaji maalum, ikiwemo Shule ya Msingi Namakonde iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa. Aidha, shilingi milioni 105.57 zimetumika kujenga uzio katika Shule za Sekondari Lindi Wasichana na Nachingwea Wasichana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaendelea kutenga fedha za ujenzi wa uzio kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na mali za shule kadiri ya upatikanaji wa fedha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved