Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 559 | 2025-06-10 |
Name
Yahya Ally Mhata
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Nanyumbu pamoja na nyumba za watumishi? (Makofi)
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu imetoa eneo Kitalu F, kiwanja namba moja kilichopo Mtaa wa Mangaka chenye ukubwa wa mita za mraba 68,682 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Nanyumbu pamoja na nyumba za makazi ya askari. Serikali inatarajia kujenga Kituo kipya cha Polisi cha Daraja B, kitakachogharimu kiasi cha fedha shilingi 802,926,788. Fedha kwa ajili ya ujenzi zitatengwa kwenye bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027. Baada ya ujenzi kukamilika, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makazi ya kuishi askari polisi, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved