Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 189 | 2025-04-30 |
Name
Daimu Iddi Mpakate
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduru Kusini
Primary Question
MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga maghala ya kuhifadhia mazao Vijijini?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026 mpaka 2029/2030 Serikali ina mpango wa kujenga maghala na vihenge yenye uwezo wa kuhifadhi tani 3,000,000 za chakula. Katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imekamilisha ujenzi wa ghala za kisasa 20 za ngazi ya kijiji zenye uwezo wa kuhifadhi tani 47,000 katika Mikoa ya Dodoma, Babati, Tabora, Kigoma, Ruvuma, Simiyu, Mtwara, Geita, Mwanza na Morogoro. ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutambua umuhimu wa maghala na vihenge katika kuimarisha usalama wa chakula nchini, kwa sasa zoezi la kufanya tathmini ya utambuzi wa ghala za umma na binafsi linaendelea. Zoezi hilo litakapokamilika litawezesha kutoa mwongozo wa namna bora ya uwekezaji wa ghala katika maeneo mbalimbali nchini.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved