Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Finance | Wizara ya Fedha | 184 | 2025-02-11 |
Name
Ameir Abdalla Ameir
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
House of Representatives
Primary Question
MHE. ABDUL YUSSUF MAALIM K.n.y. MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza:-
Je, ni miradi gani ya umwagiliaji inayofadhiliwa na mashirika ya kimataifa ambayo Zanzibar inanufaika nayo?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imenufaika na ufadhili wa mashirika ya kimataifa katika miradi ya umwagiliaji inayolenga kuongeza uzalishaji wa kilimo na kuboresha maisha ya wakulima wa Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa miradi inayotekelezwa ni Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Umwagiliaji Zanzibar, ambao unatekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Exim ya Korea ambapo umefadhiliwa kupitia mkopo wa awali wa Dola za Kimarekani 50,000,000 na mkataba wa nyongeza wa Dola za Kimarekani 18,100,000. Utekelezaji wa mradi huu umefikia 98% na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 8 Juni, 2025.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved