Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 187 | 2025-02-11 |
Name
Maryam Azan Mwinyi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Chake Chake
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:-
Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wa ujenzi wa Chuo Kikuu kishiriki cha Mwalimu Nyerere pamoja na hosteli Pemba?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo mwaka 2022, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilikipa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere eneo lenye ukubwa wa hekta 11.2 katika eneo la Mtumbi Pujini, Chakechake, Pemba kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Kampasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2023 Serikali ilianza ujenzi kwa kuanza na madarasa 10 yenye uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 1,800 ambapo ujenzi wake ulishakamilika. Serikali inaendelea na ujenzi wa awamu ya pili unaohusisha ujenzi wa jengo la utawala ambao umefikia 95% na ujenzi wa jengo la kumbi za mihadhara lenye uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 1,000 kwa mara moja ambao umefikia 60%. Serikali inatarajia kukamilisha ujenzi huu mnamo Aprili, 2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kukamilika kwa baadhi ya majengo, chuo kimeshaanza shughuli za utoaji wa mafunzo na ujifunzaji. Aidha, katika awamu zijazo Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa hosteli na miundombinu mingine katika chuo hiki. Ninakushukuru sana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved