Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 39 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 502 | 2025-06-04 |
Name
Cecil David Mwambe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ndanda
Primary Question
MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -
Je, kwa nini Serikali isiagize CAG akague URA SACCOS ya Jeshi la Polisi?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, URA SACCOSS ni chama cha ushirika kilichosajiliwa na kinasimamiwa na kukaguliwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 6 ya mwaka 2013 na Sheria Namba 10 ya mwaka 2018 ya Huduma Ndogo ya Fedha na ni mali ya wanachama ambao ni watumishi wa Jeshi la Polisi. URA SACCOSS hukaguliwa kila mwaka na Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), pia hukaguliwa na mrajisi wa vyama vya ushirika kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC). URA SACCOSS ni ushirika uliopata hati safi kuanzia mwaka 2015 hadi 2024, pia umepata tuzo ya SACCOSS bora nchini kuanzia mwaka 2021 hadi 2024, hii ni kutokana na kufuata sheria, kanuni na taratibu za ushirika na fedha na taarifa zake husomwa kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama kama matakwa ya sheria yanavyoelekeza, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved