Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 101 2016-09-16

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Katika bajeti ya 2013/2014, Serikali iliahidi kujenga Mahakama ya Wilaya ya Chunya.
Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Mahakama ya Tanzania ni kusogeza huduma za utoaji haki karibu na wananchi kwa kujenga miundombinu na kuhakikisha kwamba haki inapatikana kwa wote na kwa wakati. Katika kusogeza huduma, Serikali imedhamiria kujenga Mahakama Kuu kila Mkoa, Mahakama ya Wilaya kila Wilaya nchini na Mahakama za Mwanzo kila Kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika mwaka wa 2014/2015 tuliahidi kujenga Mahakama za Wilaya na za Mwanzo katika sehemu mbalimbali nchini ikiwemo Wilaya ya Chunya. Hata hivyo ahadi hiyo haikuweza kutekelezwa kikamilifu kutokana na upatikanaji hafifu wa fedha za maendeleo. Mahakama katika mwaka 2014/2015 ilipata asilimia nane tu ya fedha za maendeleo zilizotengwa, hivyo haikuweza kutekeleza miradi yote iliyopangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Chunya umezingatiwa katika mpango wetu wa ujenzi kwa mwaka 2016/2017.