Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 227 | 2025-05-06 |
Name
Eng. Ezra John Chiwelesa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga vituo vya kuegesha malori katika maeneo ya Nyakahura na Biharamulo Mjini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo ilitoa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kuanza matengenezo ya awali ya usawazishaji wa eneo na ujazaji wa kifusi katika maegesho ya malori Nyakahura. Aidha, katika mwaka wa fedha 2024/2025 halmashauri imetenga shilingi milioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa choo. Maegesho haya yataanza kutumika kabla ya mwezi Julai, 2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa ujenzi wa maegesho ya malori Biharamulo Mjini. Katika mwaka wa fedha 2024/2025, halmashauri imetenga shilingi milioni tano kwa ajili ya kupima na kuandaa nyaraka za umiliki wa eneo lililopatikana katika Kata ya Nyamahanga kwa ajili ya ujenzi wa maegesho hayo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved