Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 102 2016-09-16

Name

Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Primary Question

MHE. HAMADI SALIM MAALIM aliuliza:-
Je, ni kwa nini Askari wa Jeshi la Polisi hucheleweshwa maslahi yanayoendana na vyeo vyao pindi wanapomaliza mafunzo kwa ngazi mbalimbali kama vile Koplo, Sajent, Staff Sajenti, Meja na vingine?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamadi Salim Maalim, Mbunge wa Kojani, kama ifuatavyo:-
Kwanza nikiri, ni kweli kumekuwepo na matatizo ya Askari kupanda vyeo na kucheleweshewa malipo yanayoambatana na kupanda vyeo hivyo. Askari Polisi kupanda vyeo kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma na vyeo hivyo kuambatana na kuongezeka kwa maslahi kulingana na cheo walichopandishwa. Kwa mwaka 2014/2015, jumla ya askari 1,657 wa Vyeo vya uongozi mdogo walipandishwa vyeo mbalimbali na mwaka 2015/2016, Askari wapatao 3,017 walikuwa katika Vyuo vya Polisi wakihudhuria mafunzo na hivyo kupandishwa vyeo kuwa maafisa na wakaguzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwepo na ucheleweshaji kama nilivyosema wa mafao haya yanayolingana na vyeo walivyopanda kijeshi na Serikali mara zote imekuwa ikijitahidi kurekebisha mishahara ya vyeo vipya kwa haraka iwezekanavyo kwa askari waliopanda vyeo. Yapo matatizo ya kiufundi yanayojitokeza wakati wa zoezi la kurekebisha mishahara na kutokea baadhi ya askari kutorekebishiwa mishahara yao na hivyo juhudi hufanyika ili kutatua tatizo hilo mara moja na mhusika anapowasilisha malalamiko yake Polisi ama Makao Makuu.