Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 22 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 278 | 2025-05-12 |
Name
Joseph George Kakunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-
Je, lini Serikali itafikisha huduma za maji safi na salama katika shule zote za msingi na sekondari nchini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sensa ya Elimu Msingi Mwaka 2024 inaonesha kuwa shule 5,311 za sekondari zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 2,960, shule zenye maji ya visima ni 1,217 na wanaovuna maji ya mvua ni shule 1,134. Aidha, shule 20,509 za msingi zina vyanzo vya maji ya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 10,965, maji ya visima ni shule 4,966 na shule zinazovuna maji ya mvua ni 4,578.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati ya Serikali ya kufikisha huduma za maji safi na salama katika shule za msingi na sekondari nchini ni pamoja na:-
Kuhakikisha kuwa ujenzi wa shule mpya unajumuisha fedha za ujenzi wa miundombinu ya maji inayohusisha kuvuna maji ya mvua; kuunganishwa na mifumo ya mamlaka za maji na kuchimba visima; Ujenzi wa miundombinu ya vyoo unajumuisha fedha ya ujenzi wa miundombinu ya maji tiririka; na kutumia sehemu ya fedha ya ruzuku ya uendeshaji wa shule kufanya ukarabati wa miundombinu ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha shule zinakuwa na huduma ya maji safi na salama.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved