Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Madini 13 2016-11-01

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mtambula, Idunda, Maduma, Kiyowela na Idete ili wananchi waweze kufaidika na huduma hiyo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa ya kiti chako, niombe dakika moja niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kabla sijajielekeza kwenye kujibu maswali yaliyoulizwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu nawapongeza sana Waheshimiwa Wabunge jinsi ambavyo walijitoa kwenye msiba mzito wa mama yangu uliotokea wiki tatu zilizopita, nawashukuru sana na ningependa kwa ruhusa yako kwa uwakilishi wa Waheshimiwa Wabunge niwatambue wachache walioweza kufanikiwa kufika Chato kwa ajili ya msiba, lakini nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa ridhaa hiyo. Baada ya kusema hayo Mungu awabariki sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na madini, napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya kufikisha umeme nchi nzima ikiwa ni pamoja na maeneo ya vijiji vya Mufindi Kusini. Vijiji vya Kata ya Idete, Idunda, Kiyowela, Maduma pamoja na Mtambula vitapatiwa umeme kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu unaoanza Disemba mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo nilivyovitaja vya Wilaya ya Mufindi itahusisha itahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilometa 242, ujenzi wa njia ya msongo wa kilovolt 0.4 yanye urefu wa kilometa 81, ufungaji wa transfomer 24 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 3,533. Kazi inatarajiwa kuanza mwezi huu wa Disemba, 2016 na kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 11.92.