Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2016-11-02

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. JUMA H. AWESO aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Pangani ina uhitaji wa X-Ray ili kutoa huduma hiyo kwa wananchi ambao hutembea mwendo mrefu kufuata huduma hiyo Tanga Mjini:-
Je, ni lini Serikali itapeleka X-Ray katika Hospitali hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso, Mbunge wa Pangani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Pangani imeomba mkopo wa kiasi cha shilingi milioni 70 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa ajili ya ununuzi wa X-Ray mpya katika Mwaka wa Fedha 2016/2017. X-Ray iliyopo ni chakavu kiasi cha kuhitaji matengenezo kila baada ya miezi mitatu kupitia wakala wake wa Philips. Kwa sasa wagonjwa wanapata huduma ya X-Ray kupitia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri imefanya mawasiliano na NHIF kwa ajili ya kupata mkopo huo na mazungumzo yanaendelea. Aidha, Halmashauri zinashauriwa kuweka kipaumbele katika kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa X-Ray kutokana na umuhimu wake kwa afya za wananchi.