Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 3 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2016-11-03

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:-
Majibu ya Serikali ya Swali Na.1 la tarehe 6 Septemba, 2016 yanapingana na ahadi ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Magufuli aliyoitoa wakati akiwa kwenye kampeni katika Jimbo la Solwa:-
(a) Je, kwa nini Serikali inapingana na ahadi ya Mheshimiwa Rais?
(b) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali hiyo ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, Mbunge wa Solwa, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa ahadi zote za Mheshimiwa Rais unafanyika kupitia mpango wa bajeti iliyotengwa kila mwaka. Hivyo, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali haipingani na agizo la Mheshimiwa Rais na kwamba Hospitali hiyo itajengwa kama agizo lilivyotolewa. Serikali itaendelea kuweka kipaumbele na kutenga bajeti kuhakikisha ujenzi unaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyoelezwa katika jibu la msingi la Swali Na.1 la tarehe 9 Septemba, 2016, azma ya Serikali ni kuhakikisha tunakamilisha ujenzi wa Hospitali ile, ambapo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 40 kutokana na ukomo wa bajeti kwa ajili ya kuendelea na ujenzi huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejipanga kutekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais ndani ya kipindi hiki cha utekelezaji wa Ilani, ambapo tunatarajia kuongeza nguvu ya kibajeti kwa mwaka wa fedha 2017/2018.