Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 20 2016-11-02

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SALUM MWINYI REHANI (K.n.y. MHE. MACHANO OTHMAN SAID) aliuliza:-
Serikali yetu kwa muda imekuwa na uhusiano wa karibu na watu wa China, Serikali ya Watu wa China ina Ubalozi Dar es salaam na Ubalozi Mdogo huko Zanzibar:-
(a) Je, Serikali haioni kuwa sasa umefika wakati wa kufungua Ubalozi Mdogo wa Tanzania katika Mji wa Guangzhou ili kutoa huduma nzuri kwa Watanzania wengi katika mji huo?
(b) Je, ni utaratibu gani unatumika katika kuwapatia visa Watanzania ambao wameamua kuishi China zaidi ya mwaka mmoja.

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Machano Othman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, lenye vipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ina mpango wa kufungua Ubalozi Mdogo katika Mji wa Guangzhou uliopo katika Jimbo la Guangdong, China. Hatua hii imefikiwa baada ya Serikali ya China kuchagua majimbo matatu yatakayokuwa na uhusiano maalum na nchi tatu za Afrika ikiwemo Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Majimbo haya ni pamoja na Jiangsu, Zhejiang na Guangdong ambayo yamepewa maelekezo mahususi na Serikali ya China kuhamasisha makampuni kutoka kwenye Majimbo yao kuhamisha viwanda vyao katika nchi hizo na kupeleka katika nchi za Afrika, Tanzania ikiwa mojawapo. Tunaamini kwa kuanzia katika mji huo, si tu tutakuwa na fursa ya kuyashawishi makampuni ya mji huo kuja kuwekeza nchini, bali tutaweza kutoa huduma mbalimbali kwa Watanzania wanaofanya biashara katika Mji wa Guangzhou.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu uliopo unawataka Watanzania na wageni kutoka Mataifa mengine walioamua kuishi nchini China zaidi ya mwaka mmoja kuwa na kibali cha kuishi. Kibali hiki kinapatikana kwa kuwasilisha maombi kwenye Wizara inayoshughulikia na masuala ya mambo ya ndani ya China na iwapo watakidhi vigezo vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za China watapatiwa kibali cha namna hiyo.