Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 4 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 42 2016-11-04

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:-
Sera ya Elimu inasema mlinganyo wa vyoo kwa wanafunzi wa kike uwe choo kimoja kwa wasichana 20 na choo kimoja kwa wavulana 25:-
Je, utekelezaji wa Sera hiyo kwenye eneo hili ukoje?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Saleh Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hali ya sasa kuna uwiano wa choo kimoja kwa wanafunzi wa kike katika shule za msingi ni 52 na wavulana ni 54. Kwa upande wa shule za sekondari uwiano ni wanafunzi 23 kwa choo kimoja kwa wasichana na wavulana ni 25.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali imetenga shilingi bilioni 12.9 kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo 8,791 kwa shule za msingi na matundu 1,942 kwa shule za sekondari. Kazi hiyo inafanywa na Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo. Azma ya Serikali ni kuhakikisha miundombinu ya vyoo inajengwa ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia mashuleni.