Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 87 2016-11-09

Name

Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata ya Ikongosi likiwemo na Gereza la Ilupilo, Kata ya Ikweha yenye Vijiji vya Ukelemi, Uyela, Ugenza, Uhambila, Makongomi, Matelefu, Utosi pamoja na Mbugi.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mahmoud Hassan Mgimwa, Mbunge wa Mufindi Kaskazini, lililoulizwa na Mheshimiwa Chumi, Mbunge wa Mafinga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya kufikisha umeme katika maeneo yote nchini ikiwa ni pamoja na maeneo ya Vijiji vya Mufindi Kaskazini. Aidha, Vijiji vya Kata ya Ikongosi likiwemo Gereza la Ilupilo, Kata ya Ikweha, Vijiji vya Ugenza, Makongomi, Matelefu, Mbugi, Uhambila, Ukelemi, Utosi na Uyela vitapatiwa umeme kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu. Ujenzi wa mradi huu utaanza mwezi Desemba, 2016 na kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo pamoja na Wilaya nzima ya Mufindi itahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33, yenye urefu wa kilometa 242, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 81, ufungaji wa transformer 24, pamoja na kuwaunganishia wateja wa awali 3,533. Kazi hizi zitagharimu shilingi bilioni 11.92