Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 19 2017-02-01

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:-
Kumekuwa na tabia za watu kupiga watu wengine hovyo kila siku, vipigo hivyo vinafikia kiasi cha utesaji (torture) kama ilivyotokea Mbeya Sekondari kwa walimu kumshambulia mwanafunzi au mtu kumtoa macho kama ilivyotokea huko Buguruni na maeneo mengine:-
(a) Je, Serikali inaona mateso haya wanayopata Watanzania kutoka kwa Watanzania wenzao?
(b) Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuwalinda wananchi na vitendo hivi vya kikatili?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Osmund Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hivi karibuni kumekuwepo na vitendo vya kusikitisha katika nchi yetu na kwa jamii ambavyo ni kinyume cha sheria na havikubaliki. Aidha, Serikali haikubaliani na vitendo vya namna hii vinavyofanywa na mtu/watu/ kikundi kwani vitendo hivyo ni kinyume na sheria na utaratibu mzima wa haki za binadamu.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kuzuia na kuwalinda raia na mali zao. Aidha, Serikali kupitia Jeshi la Polisi hupokea taarifa za matukio mbalimbali na kuyafanyia uchunguzi wa kina na inapobainika upo ushahidi wa kutosha, mtuhumiwa huchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Nichukue fursa hii kuwaasa sana wale wote ambao wanakiuka taratibu, kanuni na sheria za nchi waache tabia hiyo mara moja. Wizara yangu haitakuwa na suluhu na mtu yeyote atakayetenda uhalifu huo.