Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 4 Public Service Management Ofisi ya Rais TAMISEMI. 44 2017-02-03

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:-
Kumekuwepo uhaba wa watumishi katika Halmashauri nyingi nchini ambao unaleta athari katika utekelezaji wa shughuli za Halmashauri kwa kutotoa huduma katika kiwango kinachohitajika.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri wataalam hasa vijana waliomaliza vyuo ambao wanazurura mitaani kwa ukosefu wa ajira?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maria Ndilla Kangoye, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jitihada za kukabiliana na upungufu wa watumishi wa umma Serikali imekuwa ikitenga bajeti ya ikama na mishahara na kutoa vibali vya ajira mpya kwa taasisi zote za umma ikiwemo Mamlaka za Serikali za Mitaa, kama ilivyo kwa sekta zote za ajira katika utumishi wa umma kwa kutegemea kiwango cha kukua kwa uchumi. Kwa kuzingatia sera za kibajeti, Serikali imetenga pia nafasi za ajira mpya katika mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo zitajazwa kwa awamu, ambapo watumshi wa umma wapatao 5,074 hadi sasa wameshaajiriwa, ikiwemo watumishi wa hopsitali mpya ya Mloganzira. Aidha, tayari Serikali imetoa kibali cha kuajiri walimu wa masomo ya hisabati, sayansi, mafundi sanifu wa maabara za shule za Serikali wapatao 4,348.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kutoa rai kwa mamlaka za ajira kutumia vizuri rasilimali watu walizonazo kwa kuwapanga watumishi wa umma kwa kuzingatia uwiano sahihi ili kuweza kukabiliana na changamoto za upungufu wa watumishi wa umma.