Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 4 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 54 2017-02-03

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:-
Wananchi wa Mloganzila waliopisha ujenzi wa MUHAS hawakulipwa fidia ya ardhi au angalau “mkono wa kwaheri” na wapo wenye madai ya „kupunjwa‟ fidia ya maendelezo:-
(a) Je, ni lini wananchi hao watapewa malipo yao kama Serikali ilivyoahidi?
(b) Je, ni kwa namna gani Serikali imeshughulikia madai ya mapunjo ya fidia ya maendeleo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Mnyika, Mbunge wa Kibamba, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya kuwalipa fidia ya hisani au mkono wa heri iliyotolewa na Serikali mnamo tarehe 20 Mei 2015 italipwa baada ya kupata fedha. Malipo haya hayajafanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia ililipa kiasi cha Sh. 8,067,904,700 kwa ajili ya fidia ya maendelezo katika ardhi kwa wananchi 1,919 katika kipindi cha mwaka 2008 mpaka 2010. Aidha, mwaka 2011 Serikali ilitenga kiasi cha sh. 1,610,374,700 kwa ajili ya fidia ya wananchi 619 waliosalia. Fedha hizi zililipwa kama fidia ya maendelezo kwa wananchi waliokuwa wamewekeza ndani ya shamba ambalo lilikuwa mali ya Serikali. Serikali haidaiwi mapunjo kwa kuwa fidia ilishalipwa kwa mujibu wa Sheria.