Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 9 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 100 2017-02-09

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-
Kufunguka kwa mawasiliano ya barabara za Tabora, Nzega, Tabora - Manyoni na Tabora - Kigoma kumeleta maendeleo ya kukua kwa Mji wa Tabora na kuongezeka shughuli za uwekezaji na ujenzi wa nyumba za makazi na biashara:-
Je, ni lini Serikali italeta Msajili wa Hati za Viwanja Tabora ili aweze kuidhinisha hati za viwanja kwa wakazi na wawekezaji kwa kuwa kwa sasa huduma hizo hazipo Mkoani Tabora?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Msajili wa Hati Msaidizi ameshateuliwa kwa kuzingatia Kifungu Na. 4 cha Sheria ya Usajili wa Ardhi, Sura Na. 334. Tangazo la uteuzi lilitolewa katika Gazeti la Serikali la tarehe 16, Desemba, 2016, Toleo Na. 52.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa Msajili Msaidizi ameshawasili kituoni. Aidha, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu mpaka sasa Wizara imeshapeleka Wasajili wa Hati katika Ofisi zote za Kanda. Rai yangu kwa Halmashauri zote nchini ni kuongeza kasi ya upimaji, upangaji na umilikishaji wa ardhi ili wananchi waweze kupatiwa hati za umiliki wa maeneo yao.