Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 8 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 88 2017-02-08

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:-

Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizoathirika kutokana na Tawala za Kikoloni na Vita ya Majimaji ni moja ya vielelezo vya athari hizo ambapo vita hiyo vilianzia Wilayani Kilwa katika Kijiji cha Nandete mwaka 1905-1907:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha waathirika wa Vita vya Majimaji wanapata fidia kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Kijerumani?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edgar Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, harakati za kupambana kivita dhidi ya ukoloni zilifanywa na makabila mbalimbali hapa nchini ikiwemo Vita vya Majimaji na nyingine nyingi. Vita hivyo vilifanywa na Watemi wa baadhi ya makabila wakiwemo Mtemi Mirambo wa Tabora, Mtemi Mkwawa wa Iringa na Chifu Abushir Bin Salim wa Uzigua Tanga. Aidha, madhila ya ukoloni kwa wananchi ni mengi yakiwa ni pamoja na utumwa, ubaguzi wa rangi, ukandamizwaji, uporwaji wa mali zetu na ardhi bora za kilimo pamoja na kuuawa kwa tamaduni zetu za asili. Haya ni baadhi tu ya madhila ya ukoloni. Maksudi ya vita za watawala wetu wa jadi ilikuwa kupinga ukoloni na kutaka kujitawala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ihakikishe kwamba Wajerumani wanawalipa fidia waathirika ni wazo zuri. Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara yangu itaiandikia rasmi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili waangalie utaratibu bora wa kufikisha kwa wahusika madai haya.