Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 60 2017-02-06

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:-
Katika Jimbo zima la Mlimba kuna kituo kimoja tu cha polisi cha Mngeta jambo linalofanya hali ya usalama kwa wananchi kuwa duni.
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya polisi katika Jimbo la Mlimba?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uhaba wa vituo vya polisi nchini na ili kuimarisha usalama nchini Serikali ina mpango wa kujenga vituo vya polisi hadi ngazi ya kata na tarafa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira hadi hapo hali ya fedha itakapokuwa nzuri na kutuwezesha kutekeleza mpango huo.