Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 67 2017-02-06

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-
Kuna mahitaji makubwa ya umeme katika Jimbo la Singida Mjini hususani katika kata za pembezoni kama vile Kisaki, Mtama, Mtipa, Mwankoko, Uhamaka, Unyambwa, Unyamikombi na Unyianga.
(a) Je, Serikali ina mpango gani kuvipatia umeme vijiji katika mwaka huu wa fedha?
(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia rasilimali ya nguvu ya upepo iliyopo Singida ili kuongeza nishati ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhan Sima, Mbunge wa Singida Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za Kisaki, Mtama pamoja na Mtipa pamoja na Mwankoko zimejumuishwa katika mradi kabambe wa REA III unaoanza mwezi Machi, 2017. Katika kazi hizi, maeneo haya yatapelekewa mradi kupitia desification, grid extension pamoja na renewable utakaoanza mwezi huo nilioutaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 105, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 126.9, ufungaji wa transfoma 31, pamoja na kuwaunganishia wateja wa awali 1,111. Kazi hii itagharimu shilingi bilioni 8.15.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa muda mrefu wa Serikali ni kutumia vyanzo mbalimbali vya kuzalisha umeme ikijumuisha upepo uliopo katika eneo la Singida ambapo katika mpango kabambe wa kuendeleza sekta ya umeme wa mwaka 2016, mradi huu umepangwa kuanza kuzalisha megawati 50 za awamu ya kwanza mwaka 2018. Mradi huu unakadiriwa kugharimu dola za Marekani 136 na utatekelezwa katika maeneo ya Kisasida, Ipungi, Mughamo na Unyankhyanya. Kampuni ya Geo Wind pamoja na Acciona wameingia exclusive agreement kwa ajili ya kipindi cha miezi minne ambayo itaishia mwezi Februari mwaka huu kwa ajili ya kujiridhisha kwa wananchi kama watakubaliana na utekelezaji wa mradi huu ili waweze kupata umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni mbalimbali binafsi zimeonesha nia ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo katika Mkoa wa Singida ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Wind East-Africa iliyojitokeza kuzalisha umeme wa megawati 50 kwa awamu ya kwanza na baadae kufikisha megawati 100. Mradi huu utatekelezwa katika eneo la Kititimo. Gharama ya mradi huu ni dola za Marekani milioni 264.77.