Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 10 2017-04-05

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza:-
Wilaya ya Mlele haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Mlele?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ni miongoni mwa vipaumbele vinavyowekwa na Halmashauri yenyewe. Kwa sasa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele imepanga kuboresha Kituo cha Afya cha Inyonga ili kiweze kutoa huduma zenye hadhi ya Hospitali ya Wilaya katika kipindi cha mpito kabla ya kujenga Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo hicho kwa sasa kina wodi nane zenye uwezo wa kulaza wagonjwa 98 kwa siku, jengo la wagonjwa wa nje, jengo la utawala lenye ofisi sita, stoo ya dawa, chumba cha maabara, chumba maalum cha upasuaji chenye vifaa vyote, mfumo wa maji safi na majitaka katika hospitali na matundu nane ya vyoo vya nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazoendelea ni ujenzi wa jengo la upasuaji ambalo limefikia hatua ya lenta na jengo la kuhifadhia maiti (mortuary) ambalo limefikia hatua za umaliziaji. Ujenzi wa majengo hayo umeshagharimu shilingi milioni 418 na kazi inaendelea.