Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2017-04-05

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA Aliuliza:-
Wilaya ya Serengeti ina Mbuga ya Wanyama ya Serengeti inayovutia watalii wengi duniani lakini inakabiliwa na uhaba wa maji.
Je, ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji kutoka Bwawa la Manchira kwenda Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mugumu na vijiji vya jirani utakamilika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji Mji Mdogo wa Mugumu utakamilika na kuanza kutoa huduma ifikapo mwezi Juni, 2017. Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.49 kupitia Mkandarasi M/S Pet Cooperation wa Kahama kupitia Mamlaka ya Maji ya Mkoa wa Mara. Utekelezaji wa mradi umekamilika kwa asilimia 62.5 ambapo mkandarasi ameshalipwa shilingi milioni 933.8.