Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 13 2017-04-05

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:-
Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika.
Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Sera mpya ya Nishati ya mwaka 2015 na Sera ya Gesi Asilia ya mwaka 2013 zinalenga kutoa fursa ya rasilimali ya gesi asilia kuwanufaisha Watanzania wote wakiwemo wananchi inapopatikana rasilimali hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika hadi sasa kuna miradi miwili inayosafirisha gesi asilia kutoka Mtwara na Lindi hadi Dar es Salaam. Miradi hiyo ni mradi wa kusafirisha gesi kutoka Mtwara na Lindi hadi Dar es Salaam uliokamilika mwaka 2015 na mradi wa Songas uliokamilika mwaka 2004. Gesi inayochakatwa inasafirishwa kwa bomba kwa maeneo mbalimbali nchini yakiwemo kwa ajili ya maeneo ya Mtwara, Lindi, Mkuranga na Dar es Salaam. Visima viwili vya gesi asilia katika eneo la Mnazi bay vimetengwa rasmi kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Lindi na Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na gesi asilia kutoka Lindi na Mtwara kutumika kuzalisha umeme kwa asilimia 50 pia gesi hiyo inatumika katika kusambaza gesi majumbani na viwandani katika maeneo mbalimbali. Kwa sasa Serikali kupitia Shirika la Maendeleo la Taifa (TPDC) inatekeleza mradi wa kuunganisha gesi hiyo katika Kiwanda cha Dangote kilichipo Mtwara ambacho kinahitaji futi za ujazo milioni 45. Pia shirika hilo liko kwenye majadiliano na kiwanda cha URANEX kinachotarajia kujengwa Mkoani Lindi ili kuweza kuunganisha gesi asilia hiyo.