Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 1 2016-04-19

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:-
Katika Jimbo la Ulyankulu, Kata za Milambo, Igombemkulu na Kamindo bado hazijafanya uchaguzi:-
Je, ni lini Kata hizo zitafanya uchaguzi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU (MHE. DKT. ABDALLAH S. POSSI) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Peter Kadutu, Mbunge wa Ulyankulu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya Uchaguzi kupitia Tangazo la Serikali Na. 295 la Tarehe 23 Julai, 2015 ilitangaza jumla ya Kata 3,946 kwamba ndizo zitakazoshiriki uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara katika uchaguzi uliofanyika mwezi Oktoba, 2015. Kata za Kamindo, Igombemkulu na Milambo hazikujumuishwa katika orodha hiyo kwa kuwa ni maeneo mapya yaliyowasilishwa na Serikali baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa imekamilisha maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba 2015.
Vilevile zoezi la utoaji uraia (naturalization) na utangamanisho (intergration) kwa baadhi ya wakimbizi bado linaendelea katika maeneo hayo. Zoezi hilo litakapokamilika taratibu za kisheria zilizopo zitazingatiwa kabla ya kufanya uchaguzi katika maeneo husika.