Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 4 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 30 2017-04-10

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliluliza:-
Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano kumekuwa na mabadiliko makubwa ya uendeshaji wa shughuli za Bunge kwa kupunguza muda. Bunge sasa hukaa kwa siku 10 hadi 12 tu jambo ambalo linasababisha muda wa kuchangia na Mawaziri kujibu hoja kuendelea kupunguzwa hadi kufika dakika tano tu kitu ambacho kimepunguza kabisa ufanisi wa chombo hiki muhimu chenye majukumu muhimu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuliwezesha Bunge
kufanya shughuli zake kwa ufanisi kwa kuliongezea bajeti?

Name

Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Serikali kuliwezesha Bunge kufanya shughuli zake kwa ufanisi ni kwa kutoa fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali kwenda kwenye Mfuko wa Bunge Fungu namba 42 kwa kuzingatia bajeti iliyoidhinishwa na Bunge, taarifa ya utekelezaji ya Mfuko wa Bunge na hali ya upatikanaji wa fedha. Kifungu cha 45(b) cha Sheria ya Bajeti kinatuelekeza tufanye hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa msingi huo, katika mwaka wa fedha 2016/2017, Mfuko wa Bunge uliidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 99 na hadi Februari, 2017 jumla ya shilingi bilioni 62.6 sawa na asilimia 68 ya bajeti ya mfuko huo zilitolewa. Serikali inaahidi kutoa fedha zote zilizobaki kwenye bajeti ya fungu hili yaani shilingi bilioni 8.3 kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi bilioni 6.7 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kabla ya tarehe 30 Juni, 2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka ujao wa fedha, Serikali imeongeza bajeti ya Mfuko wa Bunge kutoka shilingi bilioni 99 mwaka 2016/2017 mpaka shilingi bilioni 121 mwaka ujao wa fedha.