Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 63 2017-04-18

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO Aliuliza:-
Jimbo la Njombe lina Mahakama ya Mwanzo moja tu iliyopo Njombe Mjini. Je, Serikali ipo tayari kukarabati Mahakama za Mwanzo za Mahenye na Igominyi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo jirani?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Sheria na Katiba, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, moja ya changamoto kubwa zinazoikabili Mahakama ni uhaba na uchakavu wa miundombinu. Sehemu nyingi nchini hazina majengo ya Mahakama na baadhi ya majengo yaliyopo ni chakavu na ni ya muda mrefu. Aidha, ni kweli kwamba Mahakama za
Mwanzo za Igominyi na Mahenye ni chakavu sana kiasi cha kushindwa kuendelea kutoa huduma.
Mheshimiwa Spika, mpango uliopo ni kujenga majengo mapya na siyo kukarabati yaliyopo, hasa ikizingatiwa kuwa majengo haya yapo kwenye hifadhi ya barabara. Ni kweli Mahakama hizi zinahitajika sana na ni moja ya miradi ya kipaumbele katika ujenzi wa Mahakama
za mwanzo katika Wilaya ya Njombe. Katika Mwaka wa Fedha 2016/2017 kipaumbele ni ujenzi wa Mahakama ya Mkoa na kwa mwaka 2017/2018 imepangwa kujengwa Mahakama ya Mwanzo Mahenye-Uwemba; na Mahakama ya Mwanzo Igominyi imepangwa kujengwa katika mwaka 2019/2020 kulingana na upatikanaji wa fedha.
Pamoja na hayo, Mahakama imeshapata nafasi katika Ofisi ya Kijiji cha Uwemba kwa ajili ya kuendesha shughuli za Mahakama ya Mwanzo Mahenye ili huduma iendelee kutolewa wakati mipango ya ujenzi inaendelea.