Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 74 2017-04-19

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA Aliuliza:-
Matatizo ya mipaka kati ya wanakijiji na maeneo ya hifadhi husababisha migogoro kati ya wanakijiji na watumishi wa hifadhi.
Je, Serikali inachukua hatua gani kurejesha mahusiano kati ya watumishi wa hifadhi na wananchi?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba matatizo ya mipaka kati ya vijiji na maeneo ya hifadhi mara kadhaa imesababisha migogoro kati ya wananchi na wahifadhi na wakati mwingine hata kusababisha maafa katika baadhi ya maeneo.
Wizara yangu imeendelea kuchukua hatua mballimbali katika kudumisha na kuboresha mahusiono baina ya wananchi na wahifadhi zikiwemo:-
(a) Kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi na faida zake na kuwakumbusha wahifadhi juu ya umuhimu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na utaratibu.
(b) Kusaidia kuimarisha uwezo wa usimamizi wa maliasili katika ngazi za vijiji na Wilaya ikiwemo kuhamasisha uanzishwaji wa Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori (Wildlife Management Areas – WMAs) na kuimarisha zilizopo.
(c) Kuhakikisha wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopatikana na hifadhi wanafaidika na faida zitokanazo na uhifadhi katika maeneo yao kwa mujibu wa kanuni na taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itaendelea kushikiana na wadau mbalimbali katika kutekeleza sera taratibu za uhifadhi shirikishi ili kuboresha uhifadhi na kudumisha mahusiano na mashirikiano kati ya wahifadhi na wananchi.