Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 6 2016-04-19

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA aliuliza:-
Wananchi wa Ludewa wamekuwa wakisikiliza mipango ya Serikali juu ya miradi mikubwa ya Makaa ya Mawe, Mchuchuma na Liganga ambapo kumekuwa na mipango mingi ambayo kwa sasa inaonekana kutekelezwa:-
(a) Je, ni lini wananchi walioachia ardhi yao kupisha miradi hiyo watalipwa fidia?
(b) Je, ni lini miradi hiyo inatarajiwa kuanza?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deogratias Francis Ngalawa, Mbunge wa Ludewa lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, miradi ya makaa ya mawe ya Mchuchuma na Liganga inasimamiwa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji lakini inafanywa hivyo kwa kupita Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC). Miradi hii inaendelezwa kwa pamoja kwa maana ya (Intergrated Projects) kati ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) lenye asilimia 20 ya hisa na Kampuni ya Sichuan Hongda (Group) Company Limited ya China yenye hisa asilimia 80 kupitia kampuni ya ubia Tanzania China International Mineral Resources Limited (TCIMRL).
Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa leseni za uchimbaji mkubwa SML namba 533/2014 ya tarehe 09/10/2014 katika eneo la Liganga lenye ukubwa wa kilomita za mraba 30.41. Lakini SML ya pili namba 534/2014 ya tarehe 9/10/2014 katika eneo la Mchuchuma lenye ukubwa wa kilomita za mraba 25.46. Leseni hizi zilitolewa kwa kipindi cha miaka 25 na zitaisha muda wake tarehe 08/10/2039.
Mheshimiwa Spika, Kampuni ilifanya uthamini wa mali za wananchi walioko ndani ya maeneo ya miradi ambao walitakiwa kupisha shughuli za utekelezaji wa miradi mwezi Agosti, 2015 na kuridhiwa na Mthamini Mkuu wa Serikali mwezi Agosti, mwaka huo huo. Mpango wa kulipa fidia unatarajiwa kuanza mwezi Juni, mwaka huu chini ya usimamizi wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
(b) Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi unatarajiwa kuanza Machi, 2017 na kukamilika mwezi Julai, 2020 na utafanywa hivyo chini ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.