Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 12 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 99 2017-04-25

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:-
Uwanja wa mpira wa miguu Lindi ulijengwa tangu mwaka 1957 wakati wa ukoloni wa Gavana Sir Edward Twining na mpaka leo haujafanyiwa maboresho.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuukarabati na kuwa wa kisasa ukizingatiwa kwamba uwanja huo ulikuwa ukitumika kwa ajili ya michezo ya Afrika Mashariki?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge Viti Maalum. kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli uwanja wa mpira wa miguu wa Lindi (Ilula) ni mkongwe ulijengwa wakati wa ukoloni wa Mwingereza na unahitaji ukarabati ili kuufanya kuwa wa kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Maendeleo ya Michezo inahimiza kila taasisi yenye kiwanja au viwanja vya michezo kuvitunza viwanja hivyo ili viweze kudumu. Uwanja huu upo chini ya Halmashauri ya Lindi kama ilivyo kwa viwanja vingine vingi vilivyoko chini ya Halmashauri hapa nchini. Wizara yangu inashauri Halmashauri ya Lindi kuangalia uwezekano wa kuufanyia ukarabati uwanja huo kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali pamoja na wananchi wa Lindi wakiongozwa na Waheshimiwa Wabunge.
Aidha, Wizara yangu itakuwa tayari kutoa ushauri wa kitaalamu ili kusaidia kukarabati uwanja huo na kuufanya kuwa wa kisasa na kutumiwa na wanamichezo wengi zaidi wa Mkoa huo na Taifa kwa ujumla.