Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 12 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 102 2017-04-25

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-
Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC) lililokuwa na matawi karibu nchi nzima na assets mbalimbali lilibinafsishwa kutokana na sera ya ubinasfishaji.
(a) Je, ni matawi mangapi yamebinafsishwa na mangapi yamebaki mikononi mwa Serikali?
(b) Je, Serikali imepata fedha kiasi gani kutokana na ubinafsishaji huo?
(c) Kati ya matawi yaliyobinafsishwa ni mangapi yanaendeshwa kwa ubia wa Serikali?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale, lenye vipengele (a) (b) na (c) kama ifuatavyo:-
(a) Idadi ya matawi ya Shirika la Taifa la Usagishaji yaliyobinafsishwa ni 22 na yaliyobaki mikononi mwa Serikali ni matano;
(b) Katika kubinafsisha mali za NMC Serikali imepata fedha kiasi cha shilingi 7,491,611,000; na
(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika matawi yaliyobaki hakuna tawi linaloendeshwa kwa ubia kati ya Serikali na mwekezaji. Matawi hayo kwa sasa yanasimamiwa na Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko. Hata hivyo, tawi la NMC - Arusha maarufu kama Unga Limited limekodishwa kwa Kampuni ya Monaban Trading Company Limited.