Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 18 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 150 2017-05-05

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED aliuliza:-
Kwa mujibu wa Ibara ya 19(1) ya Katiba ya nchi, kila
mtu anayo haki na uhuru wa kuamini dini aitakayo, lakini pia chini ya Ibara ya 15(1) na (2) ya Katiba ni lazima sheria zifuatwe.
Je, ni kwa nini wanawake wa kiislamu wanapovaa hijabu nikabu wanavuliwa na Maafisa Usalama wanaume?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima Ali Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifutavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo kweli kuwa wanawake
wa kiislaamu wanapovaa hijabu na ama nikabu wanavuliwa na maafisa wanaume wa Jeshi la Polisi. Aidha, Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazoliongoza Jeshi hilo na kwa mujibu wa PGO 103(1) ambayo inasema malalamiko yote dhidi ya Polisi lazima taarifa itolewe mara moja kwa Mkuu wa eneo na hatua za uchunguzi upelelezi ifanyike kikamilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaombe wananchi hususani wanawake, pindi wanapofanyiwa vitendo kama hivyo, kupeleka malalamiko yao polisi au kwenye mamlaka nyingine husika ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.