Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 18 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 154 2017-05-05

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO (K.n.y MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO) aliuliza:-
Hivi sasa yapata miaka 11 utafiti wa mafuta na gesi katika mwambao wa Ziwa Tanganyika kwenye maeneo ya Kigoma, Rukwa na Katavi umefanyika au unaendelea kufanyika.
(a) Je, ni nini hali ya utafiti huo?
(b) Bonde la Mto Malagarasi nalo limefanyiwa utafiti
wa mafuta na gesi; je, hali ya utafiti huo ikoje?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Nicodem Nsanzugwanko, Mbunge wa Kasulu Mjini, lililoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Kabwe Zuberi Zitto, Mbunge wa Kigoma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni ya Beach Petroleum
ya nchini Australia ilianza kufanya utafiti wa mafuta na gesi Kusini mwa Ziwa Tanzanyika tangu mwaka, 2010. Kampuni hiyo ilifanya utafiti na kukusanya data ambazo kimsingi ziliwezesha kupatikana taarifa za uchunguzi pamoja na utafiti. Kampuni hiyo imeshindwa kuanza kuchimba gesi kwa sababu zifuatazo:-
Kwanza kabisa ni kwa sababu ya kupanda kwa gharama za uwekezaji, lakini pia kupanda na kushuka kwa bei za mafuta duniani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 10 Oktoba, 2016, Serikali za Tanzania na DRC ziliingia makubaliano ya (MoU) ya kufanya utafiti wa mafuta na gesi pamoja katika Ziwa Tanganyika. Maeneo makubwa ambayo yamekubalika kufanyiwa kazi ni pamoja na kutathmini kwa pamoja data za kijiolojia pamoja na kijiofizikia ili kutambua ukubwa wa mashapo ambayo yatavuka mpaka, vilevile kuandaa jinsi zitakavyofanya kazi kwa ushirikiano. Nchi za Burundi na Zambia nazo zimeomba kuingizwa katika makubaliano hayo ili kufanya utafiti katika ziwa lote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Motherland Industries ya nchini India iliingia ubia na Serikali kupitia TPDC kufanya utafiti wa mafuta na gesi asilia katika eneo la Bonde la Mto Malagarasi mwaka 2012. Kufuatia kushuka kwa bei ya mafuta duniani tangu wakati huo, kampuni imeshindwa kukamilisha majukumu yake ya kazi kama ilivyokubalika kwenye mkataba wa Production Sharing Agreement, kutokana na hatua hiyo, Serikali inakusudia sasa kurudisha eneo hilo kwa ajili ya utangazaji na wawekezaji wengine wapya.