Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 158 2017-05-08

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Halmashauri ya Lushoto ina mzigo mkubwa wa kulipa mishahara ya watumishi ambapo inatumia zaidi ya shilingi 28,000,000 kila mwezi kulipa mishahara ya watumishi ambao kimsingi mishahara yao ilipaswa kulipwa na Hazina kupitia Utumishi.
Je, ni lini Serikali itawatua wananchi wa Lushoto mzigo huu?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, nakushukuru na napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri za Wilaya wapo watumishi wanaolipwa kutoka Serikali Kuu na wapo watumishi wanaolipwa kutoka katika vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmshauri husika (own source). Utaratibu huu ulianzishwa baada ya kuonekana kuwepo kwa mahitaji maalum yanayowasilishwa na waajiri kutaka kuwaajiri watumishi wa ziada tofauti na ukomo wa bajeti ya mishahara ya Serikali.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kuna jumla ya watumishi 116 ambao waliajiriwa katika utaratibu huo wa mapato ya Halmashauri (own source) kwa kuwa Halmashauri hiyo iliona inaweza kumudu gharama za kuwalipa mishahara kutokana na vyanzo vyake vya mapato ya ndani.
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa wito kwa Halmashauri zote kuzingatia uwezo wao kabla ya kuamua kuajiri watumishi kwa kutumia vyao vyao vya mapato.